Mwanamasumbwi maarufu duniani kutoka Marekani, Floyd Mayweather ameamua kuliamsha bifu na swahiba wake wa zamani 50 Cent hii ni baada ya rapper huyo kumuandamana Mayweather kwenye mitandao ya kijamii.

Mayweather akitema nyongo kwenye ukurasa wake wa Instagram amefunguka kuwa 50 Cent kwa sasa anahasira na kila kijana yeyote maarufu na mwenye pesa hii ni kutokana na mpenzi wake wa zamani kukataa kurudiana naye,”Tunajua kwa sasa una hasira sana na kila mtu baada ya mzazi mwenzio wa zamani kukataa kurudiana na wewe, kumbuka yule mtoto uliyezaa naye ni damu yako lakini hujali“.

